Search This Blog

Tuesday, 23 October 2018

HOLLYWOOD PRIMARY SCHOOL YAONGOZA KIMKOA MATOKEO YA DARASA LA SABA 2018

Katibu Mtendaji wa Baraza la mitihani Charles Msonde ametangaza matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi huku kukiwa na ongezeko la ufaulu katika masomo ya Maarifa ya jamii, Sayansi, Hisabati na Kiingereza na ufaulu wa  somo la Kiswahili umeshuka ukilinganisha na wa mwaka jana.
Mkoa wa Dar es Salaam umeongoza kwakufanya vizuri kati ya mikoa 10 bora kitaifa kiufaulu kwa kuwa na watahiniwa waliopata alama nyingi kwenye masomo matano. Ukifuatiwa na Geita, Arusha, Kilimanjaro, Kagera, Mwanza, Iringa, Mtwara, Katavi na Njombe.
Ambapo Baraza hilo pia limefuta matokeo yote ya wanafunzi 357 waliobanika kuhusika na udanganyifu na kuzuia kutoa matokea ya watahiniwa 120 ambao walikuwa wakiumwa na watafanya mtihani mwaka 2019.
Kwa mujibu wa NECTA, ufauli katika masomo ya English Language, Maarifa ya Jamii, Hisabati na sayansi umepanda kwa asilimia kati ya 4.03 na 11.92 ukilinganisha na mwaka jana, Huku ufaulu katika somo la Kiswahili ukishuka kwa asilimia 1.44.
Kwa mwaka huu, watahiniwa wavulana 27,559 ikiwa sawa na 6.17% wamefaulu kwa kupata daraja ‘A’ huku wasichana 19,781 ikiwa ni sawa na 3.98% Aidha waliopata daraja ‘B’ wavulani ni 145,075 sawa na 32.46% na wasichana wakiwa jumla yao 136,166 sawa na 27.47%.
Baraza hilo pia limewatangaza walimu na maafisa waliohusika katika wizi wa mitihani ya darasa la saba pamoja na kufanya udanganyifu. NECTA imesema chimbuko la wizi lilipoanzia katika kituo teule cha kuhifadhia mitihani cha Nyanduga Rorya Mkoani Mara.

Shule ya Hollywood primary school imekua ya Kwanza kati ya shule 28 kiwilaya na ya KWANZA kati ya shule 155 kimkoa na Nafasi ya shule kitaifa ni 68 kati ya shule 6726 huku wanafunzi walio tahiniwa kufanya mtihani idadi yao ikiwa ni wanafuzi 24 tu. 
Mungu ni mwema karibu shule ya Hollywood kwa mafanikio ya mtoto wako.
Mawasiliano Zaidi Mkurugenzi wa shule 0758-38-08-03.

MATOKEO YA DARASA LA SABA HOLLYWOOD PRIMARY SCHOOL HAYA HAPA CHINI

http://41.59.85.99/psle/results/shl_ps3103144.htm
http://41.59.85.99/psle/results/shl_ps3103144.htm

MATOKEO YA DARASA LA SABA 2018-2019

Baraza la Mitihani NECTA limetangaza matokeo ya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi (darasa la saba) ambapo matokeo yanaonyesha ongezeko la ufaulu kwa asilimia 4.76% tofaiti na ufaulu wa 2017 ambao ulikuwa asilimia 72.76%

Dk. Charles Msonde amesema katika tathmini ya awali kiwango cha ufaulu kimepanda kwa asilimia 4.9% ikilinganishwa na 2017, amesema pia kiwango cha ufaulu wa somo la Kiingereza uko chini sana tofauti na masomo mengine, (-50%)

Baraza la Mitihani nchini limewafutia matokeo watahiniwa 357, waliobainika kufanya udanganyifu kwenye mitihani iliyofanyika mwaka huu 2018

"Baraza limezuia kutoka matokeo ya watahiniwa zaidi 100 kutokana na kuugua kipindi cha mtihani na kuwapa fursa ya kufanya mtihani huo mwaka 2019" Dk. Charles Msonde.
Kuona matokeo hayo | Fungua link zifuatazo

http://41.59.85.99/psle/psle.htm
http://41.59.85.99/psle/psle.htm
http://41.59.85.99/psle/psle.htm
http://41.59.85.99/psle/psle.htm

Monday, 1 October 2018

MAHAFALI YA KWANZA HOLLYWOOD ENGLISH MEDIUM PRIMARY SCHOOL

Pongezi za dhati kwa mkurugenzi wa Jumuiya ya Hollywood ikijumlisha shule ya msingi na sekondari Mstaafu Ndugu Izyasi A. Kameka, Hollywood primary school ipo katika mji mdogo wa mlowo ambao uko katika halmashauri ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe.
Ni miaka kumi toka shule ya secondary imefunguliwa na mwaka wa kwanza kwa mahafali ya kwanza shule ya English medium iliyoko mkoani Songwe Tanzania.
Mahafali hiyo ilifana sana furaha kutoka kwa wazaz Waalimu na wanafunzi waagwa.
Mkurugenzi wa shule ya Hollywood English medium Primary School Mstaafu Ndugu Izyasi A. Kameka katika sherehe hiyo pembeni yake ni Mwalimu Mkuu sekondari Hollywood Ndgu Issa Mwakasendo.

  Shule ilianzishwa mwezi January 2012 kisha kupata usajili MB.04/7/006 pamoja na maerekebisho yake mwaka 2018 ya kupewa EM.15887. 


Mwalimu mkuu Shule ya msingi Hollywood Ndugu Abraham Ntengwi akitoa risala siku hiyo.
Akisoma risala Mwalimu mkuu wa shule alisema "Taaluma ya shule mpaka sasa ni nzuri kwani hakuna mwanafunzi yeyote asiye jua kusoma, kuandika na kuhesabu kuanzia darasa la kwanza mpaka la saba. Pia shule imeshiriki mitihani ya upimaji darasa la nne kitaifa kwa miaka mitatu, kuanzia 2015, 2016 na 2017"





 Mgeni Rasmi siku hiyo Meneja wa uwanja wa Ndege wa Songwe airport  Pius J . Kazeze akihutubia katika sherehe hiyo.


MATOKEO YA SHULE
1. 2015 - Shule ilishika nafasi ya kwanza katika wilaya ya Mbozi na nafasi ya tatu kwa mikoa miwili ya Mbeya na Songwe.
2. 2016 - Shule ilishika nafasi ya kwanza kwa wilaya ya Mbozi na nafasi ya Kwanza kwa mkoa wa Songwe baada ya kutenganishwa na Mbeya.
3. 2017 - Shule ilishika nafasi ya kwanza kiwilaya na kufanya iendelee kushika rekodi yake bila kutetereka.
Katika sherehe hiyo waliagwa wanafunzi ishirini na nne(24) waliohitimu elimu ya msingi katika shle hii kwa mara ya kwanza. Walianza darasa la kwanza mwaka 2012 jumla wakiwa 25 kati yao wavulana 17 na wasichana 8. Kwa bahati mbaya mwanafunzi mmoja alitoroka masomo dakika za mwisho kabisa.
Wote kwa ujumla wana nidhamu safi hali iliyo washangaza hata wasimamizi na walinzi wakati wanafanya mitihani yao ya kuhitimu elimu ya msingi, kuanzia mtihani wa kwanza mpaka mtihani wa somo la mwisho hakuna hata mtoto mmoja alliye omba ruhusa ya kutoka nje kujisaidia. Ilikua wakiingia ni kazi tu mpaka mda wa mtihani ukikamilika ndipo wanatoka nje. Ama kwa hakika vijana hawa ni kizazi bora cha shule yetu.



 Waalimu wa wahitimu Mkono wa kushoto Madam Invyolata (Mwalimu wa Kiingereza) kulia na Madam Secilia (Mwalimu wa Kiswahili).



 HABARI PICHA.










Hitimisho Mwalim mkuu wa shule aliwashukuru waalimu na wazazi kwa ushirikiano na shule kwa ujumla. Pia alimshukuru mgeni rasmi kwa kuja kwa kuthamini mualiko wa kuja kujumuika pamoja na kutambua majukumu mengi aliyo nayo.

KWA MAWASILIANO ZAID ILI KUPATA NAFASI YA MWANANO AMA NDUGU KUJIUNGA NA SHULE YETU



Mkurugenzi wa shule ya secondary Hollywood Mlowo mkoani songwe





    0758-38-08-03




   0756 06 16 99


Mwalimu Mkuu
   
   0755-33-67-55



AHSANTE UNAKARIBISHWA SANA NA MWENYEZI MUNGU AKUBARIKI.